Sunday, August 10, 2008

IJUE SIRI YA GIRLFRIEND NA GIRLFRIEND -2

UPENDO NI NINI?
Mara nyingi vijana hudanganyana kwa kuambiana nakupenda lakini hawajui nini maana halisi ya upendo au wakati mwingine wanakuwa na upendo wa kinafiki. Upendo ni hali ya ndani ya moyo au nafsi na huelezwa kwa maneno na kwa matendo makuu mazuri yafanywayo kutoka ndani ya moyo. Upendo hauangalii gharama za kufanya tendo la upendo. Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele”

Kiasi cha upendo uliokuwamo ndani ya Mungu kwa mwanadamu, ndiyo uliomfanya Mungu kuwa tayari kumtoa mwanawe, tena wa pekee, maana yake hakuwa na mwingine lakini alimtoa kwa ajili ya uzima wetu. Kiasi cha upendo uliokuwamo ndani ya moyo wa Ibrahimu, alivyompenda Mungu ndiyo uliomfanya Ibrahimu kuwa tayari kumtolea Mungu mwamawe Isaka awe sadaka ya kuteketezwa, japo alikuwa ni mwana pekee tena aliyempata uzeeni. Si jambo rahisi lakini upendo hauhesabu gharama iliyopo katika kutenda. Maana upendo huambatana na imani ndani ya mtu. 1 Korintho 13:4-8 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu, hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wowote;…”

Kiasi cha upendo uliokuwamo ndani ya Yesu kwa mwanadamu, ulimfanya Yesu kuwa tayari kuutoa uhai wake, akafa msalabani kwa ajili yetu. Sasa mpendwa msomaji unaweza ukaelewa nini maana ya halisi upendo. Wenzetu husema ‘To love is a very great responsibility’ Siku hizi watu wengi hutumia neno nakupenda ili kukidhi haja ya tamaa zao, hawana upendo ila ni unafiki mtupu umejaa ndani mwao. Pendo lisiwe na unafiki….
SHETANI HUTUMIA MANENO MAZURI
Mara nyingi Shetani hutumia maneno mazuri, aidha yameanzishwa na Mungu au ya kibiblia ili apate kuwapoteza watu wengi. Na vijana wengi hawajui jambo hili na hivyo wengi wao hujikuta mikononi mwa Shetani na hawajui cha kufanya na mwishowe huangamizwa kabisa. Tazama mifano ifuatayo;

· Neno mpenzi lina maana nzuri ki-Biblia, 1 Kor 7:1 “Basi wapenzi wangu kwa kuwa tuna ahadi hizo na tujitakase” Maana yake anawapenda mno. Rumi 9:25 “…nitawaita watu wangu wale wasio watu wangu, na mpenzi wangu yeye asiye mpenzi wangu”

Mpenzi ni mtu yule umpendaye sana na sio upendo wa kinafiki. Si rahisi kutambua ukweli wa maneno unayoambiwa na mtu, ni lazima uwe na macho ya rohoni na ufahamu wa rohoni. Maana Roho wa Mungu ndiye ajuaye mambo yaliyo ndani ya moyo wa mtu. Wapo vijana wengi ambao huambiana ‘naomba uwe mpenzi wangu’ ila ndani yao hawana nia nzuri’ Sasa wewe utajuaje kuwa huyo anayekutaka uwe mpenzi wake ana nia mbaya na wewe na ametumia neno zuri, mpenzi au nakupenda? Roho Mtakatifu anahitajika.

· Girlfriend na Boyfriend ni maneno mazuri kabisa, huyatumia kwa maana ya kwake na kuwafanya vijana waingie kwenye mtego wake bila kujua. Ni lazima umuelewe Shetani na mbinu zake ndipo utakapoweza kumshinda kwa kutumia neno la Mungu. Maana Shetani hujigeuza, unashangaa!! Soma 2 Kor 11:14 “Wala si ajabu, maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”

Tunapotega samaki huwa tunaweka chakula chao kwenye ndoana ili wavutiwe na hatimaye wananaswa na ndoana. Vilevile katika kutega ndege au panya ni lazima uweke chakula kidoga, ambacho kitawavutia na hivyo huweza kunaswa na mtego kirahisi. Sasa na Shetani naye huweka vitu vizuri katika mambo mbalimbali kuwavutia vijana na wengi wao hunaswa na mtego kwa kuona vitu vizuri badala ya kuona mtego, maana macho yao ya rohoni hayaoni yametiwa giza . Na mara nyingi huwa hawana neno la kutosha ndani yao na hivyo hutumia akili zao kujaribu kupambanua kila kitu. Mpendwa naomba ujiulize, hivi kwa akili yako binasi bila msaada wa Mungu unaweza kujua na kutambua kuwa anayekuomba uwe mpenzi wake hakudanganyi au hana pendo la kinafiki?
JE NI VEMA KUWA NA GIRLFRIEND AU BOYFRIEND?
Vijana wengi hujiuliza swali hili. Na wengi wao huona kuwa ni vema tena yafaa, lakini hawajui maana halisi ya girlfriend na boyfriend na wala hawajui zilianzaje. Kama nilivyokueleza hapo mwanzo, Shetani hutumia maneno mazuri akiwa na maana ya kwake tofauti tena mbaya ili awateke watu. Kabla ya kulijibu swali hili na kueleza maana ya girlfriend na boyfriend na chanzo chake kibiblia ni vema ufahamu undani juu ya mapenzi na jinsi Mungu alivyoweka utaratibu wa mapenzi katika maisha ya kila mtu.

No comments: